Kuna watu wanaishi na mpaka watakufa hawajawahi kuishi maisha yao halisi mengi wanayoishi ni ya kuigiza,kuiga,unafiki,kujionyesha na kujifanya wapo sawa na wanajali zaidi wengine mpaka wanasahau yaliyo ya muhimu kwao.
*Vizuri kwenda na wakati ila jaribu kuangalia jambo hilo linakusaidia?
-Je usipolifanya utapungukiwa na nini?
-Je lina umuhimu kiasi gani maishani mwako?
*Usifanye kitu sababu wengi wanafanya ili hali hawajui mwisho wake .
-Usifanye sababu kuna mtu maarufu anafanya hivyo.
-Usifanye sababu unataka kuwa maarufu umaarufu hautafutwi huwa unakuja wenyewe kwa kutumia ule uwezo ambao Mungu ameweka ndani yako.
*Kuna watu wanafanya mambo kwa kuiga mpaka wanatia huruma ili tu waonekane na wao wanafanya kama wengine hata kama hawafurahii wanachofanya hali hiyo huitwa (unafiki)
- Wengine wanaona wasipokubaliana na mambo yanayoendelea wataonekana siyo wakisasa na labda watakosa marafiki.
-Kumbuka kujitafutia marafiki wengi ni uangamizi wa nafsi yako.
*Wengine wapo radhi waumie lakini wawapendeze wengine ili tu waonekane wapo vizuri hii ndiyo inaitwa ( ujinga)
-Hawawezi kukubaliana na ukweli wanapokosolewa kwa sababu wameshajiona wapo kwenye daraja la juu wapo radhi kupingana na ukweli ili tu waonekane washindi , watu wa hivi waepuke wasije kukujeruhi .
- Kumbuka kufanikiwa kwa mjinga kutamuua na anayekataa maonyo anataka kufa.
*Wakiona unawazuia kwenye nafasi zao wapo radhi kutunga maneno na kutengeneza story ili tu uonekane mbaya na wao waonekane wazuri.
- Usiogope kwani kila jambo lina mwisho wake na mwisho wa ubaya ni aibu.
*Usiogope kusema ukweli wakati wote hata kama watu watakuchukia lakini kuna siku watakukumbuka.
-Usijifanye kukubaliana na kila kitu kiwe uongo,ujinga,uzushi ili tu kuwapendeza watu .
*Kumbuka hakuna mtu aliyewahi kusifiwa kwa uongo na unafiki bali mtu husifiwa kwa haki na kweli.
*Hatuna maisha mengine zaidi ya haya tunayoishi hivyo acha kupoteza muda kwa mambo yasiyokusaidia.
-Acha kazi ya mshumaa kumulikia wengine huku Wewe unaendelea kuteketea.
- Ishi maisha yako.
-Kuwa mkweli kwako binafsi na kwa wengine.
-Acha uzushi,uongo na unafiki.
-Fahamu huwezi kufukia nafasi ya mwingine ata ukimuua bado damu itazungumza,hivyo usijifanye Wewe ndiyo unajua kila kitu tumia nafasi yako kwa uwezo wako za wengine waachie wenyewe.
*Usisahau kwamba huwezi kufanya kila kitu na huwezi kumpendeza kila mtu hivyo fanya sehemu yako na ushukuru Mungu kwa nafasi yako .
0 comments:
Post a Comment