Thursday, April 26, 2018

MAMBO HAYA NI MUHIMU KATIKA MAHUSIANO YOYOTE



*Usipokuwa makini  na watu unaohusiana nao kirafiki au kimapenzi  kuna uwezekano mkubwa wakachangia kuinua maono yako au kuyashusha kabisa.

*Kila uhusiano unaojihusisha nao lazima utafanya  kitu kimoja wapo au viwili kati ya hivi:
-Kukuinua
-kukushusha
-kukupoteza

*Uwe makini na watu unaotaka kuhusiana nao au waonataka kuhusiana nawe.
-Siyo wote Unaohusiana nao wanapenda kuona unafanikiwa.
-Watu unaohusiana nao kama hawakupandishi  kimtazamo basi wanakushusha.

*Usilazimishe wakuelewe  kile unachofanya maana pengine hawaoni unachokiona.

-Usiwe mwepesi kuzungumza maono yako kwa kila  aliye  karibu  yako ikiwa hujamuelewa vizuri.

-Wengi walio karibu  nawe hawataki uwazidi, wanataka mfanane.

-Watu wengi walioshindwa na kupoteza maono yao walikatishwa tamaa na watu  wa wakaribu  yao.

*Kumbuka siyo wote wanaotaka kuwa karibu nawe wana malengo mazuri kwako.
-Wengine wanataka  kuiga unachofanya.(kukuzunguka)
-Wengine wanataka kukumaliza.
-Wengine wafaidike na ulicho nacho kikiisha wataondoka(kupe)
-Wanataka  kukujua  kiu ndani(wakuaibishe).

-Wengine wanatafuta  kuchukua nafasi yako.(usaliti).

-Wengine wanataka  waonekane tu wapo na wewe.

*Tafuta kuhusiana na watu unaofanana nao kimtazamo na kitabia.
-Angalia watu waliofanikiwa kama wewe au waliokuzidi .
-Usiangalie tuu muonekano wa mtu  bali angalia maadili aliyo nayo.

Share this article :

0 comments:

Post a Comment