*Usipokuwa makini na watu unaohusiana nao kirafiki au kimapenzi kuna uwezekano mkubwa wakachangia kuinua maono yako au kuyashusha kabisa.
*Kila uhusiano unaojihusisha nao lazima utafanya kitu kimoja wapo au viwili kati ya hivi:
-Kukuinua
-kukushusha
-kukupoteza
*Uwe makini na watu unaotaka kuhusiana nao au waonataka kuhusiana nawe.
-Siyo wote Unaohusiana nao wanapenda kuona unafanikiwa.
-Watu unaohusiana nao kama hawakupandishi kimtazamo basi wanakushusha.
*Usilazimishe wakuelewe kile unachofanya maana pengine hawaoni unachokiona.
-Usiwe mwepesi kuzungumza maono yako kwa kila aliye karibu yako ikiwa hujamuelewa vizuri.
-Wengi walio karibu nawe hawataki uwazidi, wanataka mfanane.
-Watu wengi walioshindwa na kupoteza maono yao walikatishwa tamaa na watu wa wakaribu yao.
*Kumbuka siyo wote wanaotaka kuwa karibu nawe wana malengo mazuri kwako.
-Wengine wanataka kuiga unachofanya.(kukuzunguka)
-Wengine wanataka kukumaliza.
-Wengine wafaidike na ulicho nacho kikiisha wataondoka(kupe)
-Wanataka kukujua kiu ndani(wakuaibishe).
-Wengine wanatafuta kuchukua nafasi yako.(usaliti).
-Wengine wanataka waonekane tu wapo na wewe.
*Tafuta kuhusiana na watu unaofanana nao kimtazamo na kitabia.
-Angalia watu waliofanikiwa kama wewe au waliokuzidi .
-Usiangalie tuu muonekano wa mtu bali angalia maadili aliyo nayo.
0 comments:
Post a Comment