Thursday, February 9, 2017

ZINGATIA HAYA UNAPOTAKA KUCHAGUA RAFIKI SAHIHI



rafiki_wa_kweli
Kuna watu wana uchungu mioyoni,wengine wana makovu kabisa kwenye miili yao,wengine wana vilema vya Maisha.   Ukiwasikiliza watakwambia ni marafiki waliwatendea hayo.  Marafiki ni wazuri kama ukimpata rafiki sahihi.  Kuna mtu anaweza kuwa rafiki yako hata watu wanapowaona wanawaona kama ni ndugu na siyo marafiki tu.   Kuna watu wanasema hawataki marafiki marafiki zao ni wake zao au waume zao ni sawa pia kama unaweza kukaa bila rafiki haina tatizo.   
Hivi unajua kwamba maadui wengi wa watu wametokana na marafiki yaani kabla hawajakuwa maadui walikuwa marafiki.  Pia haya yanawapata sana wanawake maana wanawake huwa tunafungulia watu mioyo yetu kwa haraka Zaidi kuliko wanaume. Leo tutaangalia kwa kifupi mambo ya kuzingatia ili kuchagua rafiki sahihi.
 Angalia haya kwa huyo ambaye ni rafiki yako au unataka awe rafiki yako:
1)Je anaamini kile unachoamini? :-
-Anaamini nini kuhusu ndoa?
-Anaamini nini kuhusu mafanikio ya kiroho na kimwili?
2)Ana mtazamo gani?
-Yeye binafsi anajionaje na anawaonaje watu wengine?
-Kila wakati anapenda kuzungumzia nini?
-Huwa anakuonaje na wewe na anakuwa makini kiasi gani mnapozungumzia jambo flani linalokuhusu?
3)Ni mtu anayeshaurika?
-Unaweza kumuonywa jambo na akaelewa  bila kukasirika?
4)Je ni mkweli?
-Ni mwaminifu?
4)Anaongozana na watu wa aina gani?
Baaada Ya Kufanya Hayo
Baada ya kujiridhisha kwa yote hayo basi sikiliza moyo wako ukiona unapata  amani  juu ya huyo rafiki uliye naye au unataka kuanza urafiki naye .Ila pamoja na hayo yote ambayo utakuwa umejiridhisha zingatia haya:-
1)Usimwambie kila kitu.
 2)Mheshimu.
 3)Mpende.
 4)Mpongeze anapofanya vizuri.
 5)Msaidie na umfundishe pale asipojua.
6)Mpe pole na umtie moyo anapopitia magumu.
 7)Shida yake iwe shida yako.
 8)Inapotokea mmeshindwa kuelewena katika jambo flani basi kaeni chini mzunguze yaishe.
Si kweli kwamba hakuna marafiki wa kweli wapo, na wapo marafiki wanaofaidika na urafiki wao na wanafanya mambo makubwa, hivyo fanya uchaguzi sahihi.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment