Friday, January 27, 2017

MBINU KUU YA KUJIEPUSHA NA MATATIZO MAKUBWA MAISHANI


Wengi wana vilio mambo yamekuwa magumu,wamejaribu kutatua imeshindikana. Wengine dua na wengine wamefanya maombi  lakini bado mambo ni magumu.
Wengine wameishia kujilaumu na kulaumu wengine na kuna watu wamekata tamaa kabisa ya maisha na kuridhika na hali halisi kusema ni kawaida lakini siyo kweli.
Matatizo makubwa kwa watu na hata ulimwenguni  hayakuanza yakiwa makubwa,yalianza yakiwa madogo dogo tu na yakapuuzwa, si unajua hata mbuyu ulianza kama mchicha, na misemo mingi tu kama kama mdharau mwiba mguu huota tende. Ngoja nikuhadithie kisa kimoja kidogo:

Kulikuwa na shujaa mmoja mwenye nguvu sana.Siku moja katika mizunguko yake akatobolewa na mwiba,alipata maumivu makali sana akakaa chini akautoa.Baada ya kuutoa akashangaa! kamwiba kadogo kamemtesa hivyo , akachukia   akaurudishia na kuupigilia kabisa na nyundo.Alifanya hivyo kwa kujiambia hivi, shujaa kama mimi siwezi sumbuliwa  na kamwiba kadoogo hivi.Basi siku zikaendelea kwenda mguu ukaendelea kuvimba mwisho mguu ulioza na ikabidi akakatwe mguu.

Hapa tumeweza kuona tu kwa kifupi vile matatizo yanavyoanza na watu wanayapuuza kwa vile wanayaona ni madogo tu na wanafikiri itatokea tu yataisha yenyewe,siyo kweli hakuna tatizo linaweza kuisha lenyewe bila kutafutiwa ufumbuzi na mhusika mwenyewe.



HEBU TUANGALIE MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA KUTATUA TATIZO KABLA HALIJAWA KUBWA
-Ona vile linaweza kuleta madhara makubwa baadae.
-Usijidanganye utavumilia tu jiulize unaweza kuvumilia kwa muda gani?
-Kubali kuteseka ili tu kumaliza tatizo kabla halijakuwa kubwa.
-Fikiri vizuri je usipolitatua leo utalitatua lini?
-Watu wanaweza wasikuelewe wakati unapambana kutatua tatizo dogo leo lakini baadae watakuja kukuelewa.
-Acha kufa na tai shingoni kubali kwamba wewe ni sehemu ya tatizo na kwamba kulitatua tatizo hilo  ni bora kuliko kujionyesha mshindi wakati kiukweli una tatizo.

NIMALIZIE NA MFANO HUU.
Mtu anaanza uhusiano na mdada flani ambaye anamuona kabisa ni mvivu ama ni mchafu  ,badala amwambie mapema kabla hawajaingia kwenye ndoa, eti ananyamaza anasema nikimuoa atabadilika.Matokeo yake wanaowana ndiyo anakuwa mchafu zaidi tayari tatizo limeaanza kuwa kubwa,mume anaogopa kuleta hata marafiki zake nyumbani maana ni aibu. Matokeo yake mume anaanza kulewa na hakuwa mlevi ili tu akirudi asiuone huo uchafu,mara anatafuta mwanamke mwingine msafi ili ajifariji.
Anaanza kumsema mke wake kwa watu wa nje na marafiki Kwamba mkewe hafai lakini unashangaa kwanini si alichagua mwenyewe? Si alimpenda mwenyewe?


Hapo  ndio tunarudi na kusema usidharau tatizo au jambo ambalo unaliona dogo leo limalize mapema ama ujiandae kabisa kupambana nalo badae kama utaweza.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment