Thursday, February 16, 2017

HIVI NDIVYO UNAVYOWEZA KUSAMEHE NA KUSAHAU



Duniani kuna mambo mengi kuna watu wengi, na kila mtu ana tabia yake tofauti na mwingine .  Tabia hizi za watu tofauti zinaweza kukufurahisha au kukuchukiza.  Na katika kila mazingira kuna changamoto tofauti tofauti.  Siku zote watakaokuudhi na kukuumiza siyo watu waliopo mbali nawe ila ni wale utakaokuwa karibu nao. Wale waliokusaidia au uliowasaidia,wanaokujua vizuri na wewe unawajua vizuri.  Hawa ndiyo watu ambao usipokuwa makini watakuumiza sana na unapoanza jambo ni wepesi kukutia moyo au kukukatisha tamaa . Waha ndio hutoa pia taarifa zako kwa maadui na wanafanya hivi maana wanataka uendelee kuwa kama wao.

Tatizo la kutosamehe linaanza kwakua hukutegemea kuumizwa   
Kuna watu unawaamini kuwa wanakupenda kweli  nawe waamini kwakuwa  wanakuchekea. Ila kama ungefunguliwa mioyo yao usingeamini kama ni wao waliokuwa wakicheka.  Ni wepesi sana kujionyesha kwa nje kwamba wapo nawe bega kwa bega na wanaweza hata kujitolea vitu vingi kwa ajiji yako,wakati mwingine wanakushauri jambo linakusaidia . Basi unaweka tegemeo kwao na kuwaamini, wakati umewaamini na unawategemea ndipo unagundua  walikuwa wanafiki .  Tumeshuhudia watu wachukua maamuzi mabaya baada ya kugundua walikuwa na marafiki hewa.
Wengine wametengeneza chuki milele wana huzuni wana uchungu mioyoni mwao.  Hawaamini tena mtu yeyote,wamekuwa na hasira kila wakati.  Pamoja na dunia kuwa na watu wabaya ina watu wazuri, pia kwa hiyo usishindwe kuishi kwa amani kwa sababu ya watu wachache uliokutana nao maishani.Pamoja na kwamba walikuumiza  au waliharibi Maisha yako kabisa ,huna sababu ya kuwashikilia .  Pengine aliyekuumiza ni mpenzi,mzazi,mtoto au ndugu uliyezaliwa naye.

Zingatia haya ili uweze kusamehe.
1)Fahamu kwamba kukosea kupo na kama asingekukosesha huyo labda mtu mwingine tu usiyemjua aweza kukukosea.
2)Wewe pia unaweza kukosea hata kama siyo kosa kama hilo basi jingine tu.
3)Usipoteze muda mwingi kutafakari jinsi alivyokukosea ila tafakari,ila fikiri vile unaweza fanikiwa.
Mfano:Mtu amekusema vibaya acha kutafakari kwa nini aseme hivi? Kwani nimemkosea nini?na maswali mengine mengi kama hayo, badala yake fikiri namna gani waweza kumuepuka.
4) Usitegemee kuombwa msamaha ndiyo usamehe ,maana kuna wengine hukosea bila kujua kama wamekosea.

Faida za kusamehe.
1)Unaposhikilia jambo kwa mda mrefu kichwani utashindwa kufiri vizuri mambo ya msingi,kwa hiyo unaposamehe unaisaidia akili yako kufikiri mambo kwa wepesi Zaidi.
2)Pia utakuwa na furaha wakati wote maana hauna jambo linalokupa huzuni kila wakati.
3)Utaheshimika na hawa unaowasamehe na watakuogopa maana wao walitegemea baada ya kufanya waliyofanya ungenyong’onyea sana.

Baada ya kusamehe kumbuka haya yafuatayo:
1)usimwani sana mtu na  kumwambia kila kitu chako.
2}Pia siyo lazima baada ya kumsamehe uhusiano wenu ukawa kama zamani,maana labda hilo jambo alilokukose  huyo mtu ndiyo udhaifu wake kwahiyo mnaweza rudisha uhusiano akarudia tena kukuumiza.
3)Pia siyo wote wanaokosea wamekusudia,kuna wengine imetokea tu hata kama ni kosa kubwa unaweza kumsamehe na mkaendelea na ukaribu ikiwa alipokosea alionekana kujutia kosa lake.

Samehe tu bure ili wakati mwingine na wewe ukikosea usamehewe.    
Share this article :

0 comments:

Post a Comment