Saturday, January 14, 2017

KINYWA CHAKO KAMA CHANZO CHA MAFANIKIO MAISHANI



Mungu amemuumba mwanadamu na kumpa kinywa ili aweze kula chakula aishi na aweze kuwasiliana kupitia kinywa hicho, ila wengi wetu tumekuwa tukitumia tofauti na baadhi wanatumia vizuri.
Yale unayosema yatakutambulisha wewe ni nani na maneno yako yatakuunganisha na watu wa aina yako.Pia maneno yako yanaweza kukutenga na watu au kukuunganisha na watu.
Na kuna watu wameshindwa kufanikiwa sababu ya midomo yao,siyo lazima kuongea ikiwa huna kitu cha kusema. Usiongee tu sababu unataka kuongea.

Jiulize haya kabla hujaongea;
-kwa nini unataka kusema hayo unayosema?
-Watu watafaidikaje na hicho unachosema?
-Watu watakuelewaje baada ya kukusikia?-
-Je ni muhimu sana kusema hicho unachosema kwa wakati huo na mazingira hayo?
-Wewe binafsi utapata faida gani na hicho unachosema?
-Na ukiona haina ulazima wewe kuongea nyamaza.
-Jiulize mbona wengine hawasemi na wewe ndio unataka kusema?

Sikia hiki kisa  kuna kitu nataka ujifunze:
Kuna mwanamke mmoja alienda kwa mganga, akitaka mganga ampe dawa amuwekee mume wake maana mume wake alikuwa akichelewa kurudi nyumbani,anarudi amelewa na mke anapojaribu kumwambia mbona anafanya hivyo alikuwa akimpiga.basi mganga akamsikiliza yule mwanamke akagundua yule mwanamke anaongea sana.
Basi mganga akafikiria ni jinsi gani ataweza kumsaidia huyu mwanamke ili apunguze maneno mengi ambayo ndiyo yanampelekea mume wake kurudi usiku,huku amelewa ili asimsikie akiongea.Mganga akampa yule mwanamke majivu akamwambia hiyo ni dawa,jinsi ya kutumia sasa akamwambia afanye kazi zake mapema kabisa akimaliza aoge na kujipaka hiyo dawa kidogo mikononi na usoni kidogo ahakikishe haionekani na amsubiri mumewe,mumewe anaporudi amkumbatie na ,amshike na ile mikono aliyojipaka dawa na kumbusu na kumwambia anampenda .Baada ya hapo amtengee maji ya kuoga  akimaliza kuoga basi ampe chakula.Wanapofika kitandani ampe mapenzi motomoto.Na ikiwa atamwongelesha mumewe maneno mengi au kwa ukali basi dawa ingeharibika.Mwanamke akafanya kama alivyoagizwa na mganga mume akashangaa mbona mkewe haongei sana kama mwanzo?siku ya kwanza, ya pili , ya tatu mume akaacha pombe akaanza kuwahi nyumbani na ndoa ikawa na Amani.Akarudi kumshukuru mganga akamwambia maneno yake mengi ndiyo yaliyokuwa yakiharibu ndoa yake,basi yule mwanamke akajifunza kwamba namna  gani anafaa kuzungumza na mumewe.

Turudi kwenye mada yetu.
-Siyo lazima useme kila unachokiona au unachoambiwa au unachosikia.
-Usiseme habari za mtu ambazo hajakutuma kusema.
-Usifikiri watu walionyamaza hawazungumzi hovyo labda hawajui unachokijua au hawaoni unachokiona.
-Hakikisha unasikiliza Zaidi kiliko kusema.
-Usipende kuzungumzia jambo usilolijua vizuri maana hii itawafanya wanaokusikiliza wakudharau.
-Sema ukweli.

KUMBUKA HII SIKU ZOTE.
Mpumbavu akinyamaza katikati ya wenye hekima naye huhesabiwa pamoja na wenye hekima.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment