Sunday, April 29, 2018

AKILI UNAYOHITAJI WAKATI UPITAPO KWENYE SHIDA .



Kuna wakati unaweza kuwa unapitia  magumu ambayo hakuna anayejua ila  wewe na moyo wako tu, hali hiyo inakufanya  wakati mwingine usiwe mwenye furaha ,unakuwa  na hasira kila wakati ,hujiamini,umwamini mtu  ukiona watu wanacheka unahisi unachekwa wewe.

*Inawezekana kinachokunyima amani  ni ndoa,kukosa kazi,watoto, mchumba,biashara haina faida,kodi ya nyumba,masomo magumu ,magonjwa ,bosi mkorofi au huduma unayofanya kanisani au msikitini.

*Hicho ni kipande kidogo  tu kwenye maisha nacho kitapita,usifikiri hali  hiyo unayopitia unapitia   mwenyewe ,ni wengi  wanapitia magumu  tena labda makubwa kuliko yako.

*Tunatofautiana katika  kupokea mambo wapo wanaopitia magumu  maishani  kuliko yako ,lakini wameyapokea kawaida wana amani na maisha yanaenda.

*Vile utapokea tatizo na kuamua kulikuza kuona tatizo ni kubwa kuliko wewe na  lina  akili kuliko wewe ndivyo litakavyokuwa wakati mwingine unafikiri  labda hilo  tatizo ni jipya hakuna anayepitia  tatizo kama hilo. Kumbe ni vile tu watu hawasemi .

*Acha kuruhusu  matatizo yakuongoze na kukutawala,Acha kumwambia kila mtu matatizo yako na uwache kujidanganya kwamba una shida kuliko watu wengine.

*Mungu amempa kila mtu  akili na uwezo wa kufanya mambo,ndio tunaona vitabu vya dini vinasema Mungu alimuumba Adamu na Eva lakini hakuna mahali vitabu  vinasema Mungu akawatengenezea nyumba alijua amewapa akili ya kuwatosha kufanya mambo na alijua wakinyeshewa na mvua watatumia akili kutafuta njia ya kujikinga  ikiwa ni pamoja na kujenga nyumba.

*Acha kuhuzunika mambo unayopitia ni ya kawaida  tumia tu akili yako kufikiri namna unaweza kutatua tatizo lako ukishindwa tafuta wataalamu au watu unaowaona wamefanikiwa katika hilo jambo kutaka ushauri kwao.

*Pia achana na watu watu ambao kila wakati wanasema mambo ni magumu na hayawezekani, kwani kila jambo unalopitia  ni size yako unaweza kulitatua ......siunajua mti hulala pale ulipoangukia .... na tatizo ulilonalo unaliweza ndiyo maana limekupata wewe na siyo mwingine. Matatizo tunayopitia maishani yanatufanya  tuwe imara zaidi , wewe  shahidi hakuna mtoto wa darasa la pili anayepewa mtihani wa darasa la saba  ni kitu kisichowezekana  ni lazima atapewa mtihani wa kiwango chake alichofikia.

*Pambana kutafuta njia ya kutatua  tatizo ulilo nalo usiridhike na kubakia kusema tuu umeshazoea
-Maisha ndivyo yalivyo,  au wakati mwingine una acha kutatua tatizo linalokusumbua na unaanza kulaumu.mfano:
-Wazazi,
-Serikali ,
-Mume/mke,
-Watoto au kujihukumu mwenyewe.

  SAFARI  YA MAFANIKIONI NI SAFARI AMBAYO KILA  MTU ALIYE HAI INAMHUSU  VIKWAZO NI VINGI NJIANI PAMBANA KUVISHINDA MAANA  VIKWAZO VINAINUKA KUTAKA KUKUCHELEWESHA UFIKE KWA KUCHELEWA  NA UKATE TAMAA UAMUE KUBAKI HAPO AU URUDI ULIKOTOKA .

Share this article :

1 comments:

  1. Ukiwa umefanya kazi maisha yako yote kujenga familia na urithi, huwezi kuruhusu kivuli cha mtu wa tatu kiiharibu katika miezi michache tu. Niligundua kuwa mabadiliko ya ghafla ya tabia ya mume wangu yalikuwa kuingiliwa kiroho, si tu mgogoro wa katikati ya maisha.

    Niliwasiliana na Mystic Kakaa kwa ajili ya uingiliaji kati wa kibinafsi. Kazi yake ilikuwa ya upasuaji. Alitambua kivuli na kukiondoa kabisa bila drama yoyote ya umma. Ndani ya siku 5, umakini wa mume wangu ulirudi nyumbani kwetu na katika mustakabali wetu. Ikiwa unalinda maisha yenye thamani kubwa na unahitaji bwana anayeelewa busara, wasiliana naye kwa: dawnacuna314@gmail.com

    WhatsApp: +2349046229159

    Yeye ndiye kiwango cha dhahabu.
    Kwa uchawi wa upatanisho wa uhusiano/ndoa.

    Uchawi wa kumfanya mpenzi wako wa zamani/mwenzi wako aombe msamaha.

    Uchawi wa kumrudisha mpenzi wako/kumvutia mpenzi mpya.

    Uchawi wa kurejesha mali/pesa zilizoibiwa.

    Mabadiliko ya umbo/Uchawi wa kutoweka.

    Uchawi wa kushinda bahati nasibu/kesi ya mahakama. Na zaidi

    ReplyDelete